ABAKWA, ANYONGWA HADI KUFA NA KISHA KUINGIZWA CHUPA SEHEMU ZA SIRI HUKO CHALINZE
JAMANI jamani! Dunia imefika pabaya zaidi, Mungu asaidie. Mwanamke mkazi wa Chalinze, Mkoa wa Pwani, Moshi Rashid (43) amefanyiwa unyama uliopitiliza na watu wasiojulikana baada ya kumbaka na kumnyonga, inauma sana kwa kweli!
Tukio hilo la kutisha lilijiri usiku wa Desemba 7, mwaka huu Chalinze Kwamwarabu ambapo mwanamke huyo alikwenda kujumuika na ndugu na majirani katika mkesha wa ngoma ya kuwatoa wari siku ya Jumapili.
Mkasa huu unasimuliwa kwa majonzi mazito na mdogo wa marehemu ambaye alikuwa mshehereshaji wa shughuli hiyo ‘MC’, Siwema Rashid.
Alisema: “Mpaka sasa tunashindwa kuelewa kilichotokea maana siku ya tukio tulikuwa naye kwenye ngoma usiku. Alikuwa mchangamfu sana, aliifanya shughuli ipendeze.
“Walimbaka wakaona haitoshi wakamwingiza chupa ya soda sehemu ya siri ya mbele halafu wakamwingiza chupa ya bia sehemu ya siri ya nyuma.
Aliongeza: “Marehemu ametuachia jukumu la malezi kwa watoto wake wawili, Sikudhani Juma (18) na Ally Juma (12).”
Naye mtoto mkubwa wa marehemu, Sikudhani akisimulia kifo cha mama yake, alisema: “Nasikitika sikuweza kuuona mwili wa mama hata pale watu walipojazana na kumshangaa.
“Hata polisi na mganga mkuu wa mkoa walipofika kumchomoa zile chupa sikutaka kusogea kabisa, naamini Mungu atawaonesha jambo hao watu hapahapa duniani.”
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Yurichi Mtei akizungumzia ukatili huo alisema: “Taarifa za tukio hilo bado hazijafika kwangu kutokana na majukumu mengine ya kikazi, isipokuwa nalifanyia kazi kuhakikisha watuhumiwa wanakamatwa.”
Tukio hilo lilifunguliwa jalada kwenye Kituo cha Polisi Chalinze kwa nambaCH/RB/3767/2013 MAUAJI.
Mpaka kifo chake, mwanamke huyo alikuwa akiishi na mwanaume mmoja (jina halikupatikana mara moja lakini si aliyezaa naye watoto hao wawili). Alizikwa Jumapili iliyofuata, Chalinze.
Mungu ailaze pema peponi roho yake. Amina.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Yurichi Mtei akizungumzia ukatili huo alisema: “Taarifa za tukio hilo bado hazijafika kwangu kutokana na majukumu mengine ya kikazi, isipokuwa nalifanyia kazi kuhakikisha watuhumiwa wanakamatwa.”
Tukio hilo lilifunguliwa jalada kwenye Kituo cha Polisi Chalinze kwa nambaCH/RB/3767/2013 MAUAJI.
Mpaka kifo chake, mwanamke huyo alikuwa akiishi na mwanaume mmoja (jina halikupatikana mara moja lakini si aliyezaa naye watoto hao wawili). Alizikwa Jumapili iliyofuata, Chalinze.
Mungu ailaze pema peponi roho yake. Amina.
GPL
Posted by
Unknown

Labels:
Habari za Kitaifa
Udaku wa Tanzania
Related Articles
- HEMED 'PHD' ALA SHAVU LA KUIGIZA FILAMU ZAMBIA.
- MACHANGU NA WATEJA WAO WAKAMATWA NA OFM YA MWISHO MWAKA, BALAA.
- BAADA YA KUKAA KAMA WACHUMBA KWA MIAKA 15, MAMA TUNDA ATEMANA NA AFANDE SELE.
- CHUCHU HANS AJICHORA TATOO YA RAY, NI KUONESHA JINSI GANI MAHABA YAO YAPO JUU
- WEMA AWATIBUA FANS WAKE NA VIVAZI VYAKE VYA UTATA
- ANAETAKA KUMWOA LULU KUTOA MAHARI YA TSH LAKI 8
- Lina asaka Mimba
- NAY WA MITEGO ABAMBWA AKIWA NA LUNDO LA MABINTI, MANAIKI STYLE.
- "NILIMWANDIKIA MATONYA WIMBO WA VAILETH NA DUNIA MAPITO ILA HANA SHUKRANI" TUNDA MAN