GRACA MACHEL, MJANE WA MANDELA NA SAMORA MACHEL
Mwaka 1975 hadi 1986, Graca alikuwa mke wa Rais wa Msumbiji, marehemu Samora Moses Machel. Wakati huo, Graca alikuwa waziri wa elimu na utamaduni wa nchi hiyo.
Hata hivyo, Graca alishika nafasi ya u-first lady wa ‘Sauz’ kwa mwaka mmoja tu, 1999 mumewe hakugombea tena urais.
Kifo cha mumewe kimempa ujane mwingine unaodaiwa kutotokea duniani, kuolewa na rais, rais kufa, kuolewa na rais mwingine naye kufa.
HISTORIA YA GRACA KWA UFUPI
Graca alizaliwa Oktoba 17, 1945 katika Jimbo la Gaza nchini Msumbiji.
Alipata elimu ya msingi jimboni humo, elimu yake ya chuo kikuu aliipatia Lisbon, Ureno.
Ana watoto wawili, Malengani na Josina aliowapata kwa marehemu Machel. Hakupata mtoto kwa Mandela.