ANGALIA PICHA 5 ZA WANAFUNZI WA HOSTELI WAKIJIACHIA BAADA YA KUWA MBALI NA WAZAZI WAO



Wazazi, ni vyema kwenu kujijengea mazoea na utaratibu wa kuwa karibu na watoto wenu hasa linapokuja suala la mahusiano yao na marafiki.

Inawezekana kabisa kuharibikwa kwa mwanao kukatokana na aina ya watu anaokuwa nao karibu, kitu ambacho naamini kama mzazi usingependa kitokee kwa mwanao.
 
Utajisikiaje ukikuta aina hii ya picha ya ndugu yako....?



Read More »

MCHEKI ETOO AKIWA NA MWANAE HAPA



Cheki picha zake alipokuwa mdogo uwanjani na akicheza kabumbu.


Samuel na David baada ya Fainali ya Copa De Rey
Baba na Mwana mnamo 2007

Read More »

RAIA WAWILI NA POLISI WAWILI WAFARIKI KATIKA MAPIGANO HUKO MOROGORO


Watu watatu, akiwamo askari polisi wamefariki dunia na wengine watatu kujeruhiwa baada ya kuzuka mapambano kati ya polisi na raia katika Kijiji cha Igwati, Tarafa ya Malinyi Wilaya ya Ulanga, Morogoro.
Diwani wa Kata ya Malinyi, Said Kila aliwataja waliofariki dunia kuwa ni Leon Chikwita, Andrew Likomoka na Edson Kidunda.
Alisema mmoja wa majeruhi Idelfonce Malenga (35), hali yake ni mbaya baada ya kupigwa risasi shavuni. Majeruhi wawili majina yao hayakufahamika mara moja.
Diwani Kila alisema mauaji hayo yalitokea baada ya kundi la wakulima kuvamia Kituo cha Polisi Malinyi kushinikiza kuachiwa kwa wenzao watatu waliokuwa wanashikiliwa kwa tuhuma za kumuua mfugaji mmoja wa kijiji hicho hivi karibuni.
“Baada ya kupata taarifa za kukamatwa kwa wenzao walifika kituo cha polisi ambako, hawakuwakuta watuhumiwa hao kwani walikuwa wamehamishiwa kituo kingine,” alisema diwani huyo.
Alisema katika jitihada za kulinda kituo, polisi walitoa tahadhari mbalimbali za kuwataka wananchi hao kutawanyika ikiwamo kupiga mabomu ya machozi, lakini waliendelea kukaidi amri hiyo na badala yake walizidi kujikusanya na kukivamia na kisha kukichoma moto pamoja na gari la askari lililokuwapo. Katika shambulizi hilo, ndipo mauaji hayo yalipotokea.
Chagonja eneo la tukio
Kutokana na tukio hilo, Mkuu wa Jeshi la Polisi, IGP Said Mwema ametuma timu maalumu ikiongozwa na Kamishna wa Operesheni na Mafunzo, Paul Chagonja kwenda kuongeza nguvu katika operesheni ya kuwasaka na kuwakamata wote waliohusika na tukio hilo.
Msemaji wa Jeshi la Polisi, Advera Senso ilisema jana katika taarifa yake kwa vyombo vya habari kuwa, IGP Mwema ametoa wito kwa wananchi wa Mkoa wa Morogoro hususan, Kata ya Malinyi kuwa watulivu na kuendelea kutoa ushirikiano kwa Polisi wakati uchunguzi ukiendelea.
Chanzo cha mgogoro
Mgogoro kati ya wafugaji na wakulima wa Igwati ulianza Desemba 13, mwaka huu wakati kundi la wananchi lilipomkamata mfugaji huyo na kumpeleka katika ofisi za kijiji.
Ilidaiwa kuwa baada ya kumfikisha, mtendaji wa kijiji alimfungia mtuhumiwa huyo ofisini kwake na kuanza kuhoji sababu za wananchi kumkamata jambo ambalo linaelezwa kwamba liliwakera na kuanza kumshambulia hadi kuikimbia ofisi na kumwacha mfugaji huyo ambaye alishambuliwa na kuuawa.
Kitendo cha kukamatwa na kupigwa hadi kuuawa kwa mfugaji huyo kinadaiwa kuwa kilikuwa cha kulipiza kisasi baada ya wafugaji kuvamia nyumbani kwa Mjumbe wa Kamati ya Mazingira, Victoria Marietha na kumjeruhi vibaya kisha kufariki dunia katika Hospitali ya Lugala, Malinyi alikokuwa akipatiwa matibabu.

Read More »

Kutana na Mtoto wa Miujiza Aliyezaliwa Tarehe 11.12.13 Mida ya Saa 14:15


Mara nyingi mtoto wa kwanza wa mama yeyote huwa ni wa matukio na mambo mengi sana anapozaliwa - ila siku ambayo mtoto wa Chelsea Johnson alizaliwa ilifanya kuwa na kitu kikubwa cha ziada kukikumbuka na kwa sababu maalum kabisa.

Sio tu kwamba alikuwa kama Landon-Jonah Johnson ambaye alizaliwa mnamo December 11, 2013, ila pia alifanya timing ya ajabu kwa kuingia Duniani, hii ni baada ya mtoto huyo kuziliwa mnamo majira ya saa 14:15 hivyo kufanya siku na muda aliozaliwa kusomeka hivi 11/12/13 14:15.

Chelsea, mwenye miaka 21, kutoka Rawmarsh, Rotherham, alisema kwamba mtoto wake ni wa ‘miujiza’.

“Ni mtoto maalumu,” alisema. “Nasubiri kwa hamu kuja kumueleza kipindi atakapokuwa mkubwa, na kwamba anatambua ni aina gani ya tukio lilikuwa
.” 


Read More »

AFANDE AACHA LINDO BENKI NA KWENDA KUMKAMATA DEREVA WA BODABODA


Afande akiwa amemdhibiti dereva wa bodaboda.
Wasamaria wema wakijaribu kumbembeleza afande.
Afande akiwa…
Afande akiwa amemdhibiti dereva wa bodaboda.
Wasamaria wema wakijaribu kumbembeleza afande.
Afande akiwa amecharuka hataki kusikia cha mtu.
Afande kakomaa.



Afande aliyekuwa akilinda Benki ya NMB iliyopo Mtaa wa Samora karibu na Idara ya Habari 'Maelezo' jijini Dar, leo mchana aliacha lindo lake na kuanza kukamata bodaboda zilizokuwa zikivunja sheria za usalama barabarani kama anavyoonekana pichani akimdhibiti mwendesha bodaboda.

Read More »

ABIRIA 213 WANUSURIKA KIFO BAADA YA NDEGE YAO KUTUA KWA DHARULA KATIKA UWANJA MDOGO WA ARUSHA


Abiria 213 waliokuwa wakisafiri na ndege ya Shirika la Ndege la Ethiopia jana walinusurika kifo baada ya ndege hiyo kutua kwa dharura katika uwanja mdogo wa Arusha.
Ndege hiyo aina ya Boeing 767, ilitua saa 6.45 mchana katika uwanja huo baada ya kushindwa kutua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (Kia) kutokana na kupata pancha kwa ndege nyingine inayomilikiwa Shirika la Ndege la Tanganyika (TFC), kwenye njia ya uwanja huo.

Ndege ya Ethiopia ililazimika kuelekea Arusha na kutua kwenye uwanja huo mdogo kuweza kupokea ndege kubwa kutokana na kuishiwa mafuta.
Ndege hiyo iliyokuwa inatokea Addis Ababa, Ethiopia ikiwa pia na wahudumu 23, baada ya kutua kwenye Uwanja wa Arusha, ilinasa kwenye tope baada ya tairi lake la mbele kuvuka sehemu ambayo lami inaishia kutokana na ufupi wa njia zinazotumiwa na ndege zinapotua kwenye uwanja huo.
Jitihada za kuiondoa ndege hiyo zilishindikana jana. Ndege hiyo ilikuwa ikielekea Johannesburg, Afrika Kusini kwa kupitia Kia na Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar es Salaam.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas alisema: “Rubani amejitahidi kutua katika uwanja huu japo ni mdogo ili kuokoa maisha ya abiria kwani walikuwa hawana mafuta ya kutosha kwenda uwanja mwingine.”
Tukio la ndege hiyo kutua kwa dharura limekuja siku chache tangu ndege ya Shirika la Ndege la Precision iliyokuwa na abiria 37 kupasuka matairi manne ilipokuwa ikitua kwenye Uwanja wa KIA Jumamosi 


Read More »

CHADEMA WAZIDI KUMKAA KOONI ZITTO


Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimesema hakitashughulikia rufaa iliyokatwa na Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe, kwa Baraza Kuu kupinga uamuzi wa Kamati Kuu (CC) wa kumvua nyadhifa zake katika chama, hadi hapo itakapopitia utetezi wake na kuamua hatima ya uanachama wake katika chama hicho.
Pia kimethibitisha kupokea utetezi dhidi ya mashitaka 11 yanayohusisha usaliti dhidi ya chama na kuwachafua viongozi wakuu kupitia waraka wa mabadiliko.
Mashtaka hayo yanamkabili Zitto, pamoja na aliyekuwa Mjumbe wa CC, Dk. Kitila Mkumbo na aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Arusha, Samson Mwigamba.
Kaimu Katibu Mkuu wa Chadema, Victor Kimesera, alisema hayo alipozungumza na NIPASHE, ofisini kwake, jijini Dar es Salaam jana.
Kimesera, ambaye ni Katibu Mtendaji Ofisi ya Katibu Mkuu wa Chadema, alisema rufaa hiyo ni kitu kidogo, hivyo haiwezi kuanza kushughulikiwa na chama katika sakata la Zitto na watuhumiwa wenzake.
“Kuna (kitu) kikubwa cha mbele yake (rufaa),” alisema Kimesera akijibu swali la NIPASHE lililotaka kujua nini kinaendelea kwenye chama baada ya Zitto kukata rufaa.
 Kimesera alisema kitu kikubwa kuliko rufaa, ambacho kitaanza kushughulikiwa na chama ni maelezo ya utetezi wa Zitto na watuhumiwa wenzake.

Alisema hiyo ni kwa sababu tayari kuna hoja ya CC, ambayo inataka ijiridhishe kama Zitto na wenzake waendelee kuwa uanachama au la.

 Kwa mujibu wa Kimesera, baada ya Zitto na wenzake kuwasilisha utetezi wao, CC itaitishwa na kuyapitia na kisha itatoa maamuzi juu ya uanachama wao.
“Sasa huwezi kuongea juu ya rufaa wakati hujajua uanachama wao kwanza,” alisema Kimesera.

 Hivyo, alisema rufaa ya Zitto itaendelea kuhifadhiwa kwenye jalada hadi hapo hatua ya kwanza ya kupitia maelezo yao ya utetezi na kuyatolea maamuzi itakapochukuliwa. “Lazima twende kwa hatua. Kwa hiyo, hiyo (rufaa) imekaa,” alisema Kimesera.

 Mwanasheria wa Zitto, Albert Msando, alitaja sababu mbili za mteja wake kukata rufaa kuwa ni kukiukwa kwa taratibu za kuchukua hatua za nidhamu na sababu zilizotolewa kutokuwa sahihi.

Msando alitaja kifungu cha 6.5.6 cha Kanuni ya Uendeshaji ya chama hicho, akisema utaratibu uliotakiwa kufuatwa kabla ya kumchukulia hatua za kinidhamu kiongozi kwa mujibu wa Katiba na Kanuni ni kupewa kwanza mashtaka kwa maandishi ili apate nafasi ya kujibu.
Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe.
 Alisema kiongozi yeyote hatachukuliwa hatua za kinidhamu bila kwanza kupewa mashtaka yake kwa maandishi na mamlaka husika na kupewa nafasi ya kujibu mashtaka kwa maandishi.

Alitaja  ibara ya 5.4.3 na 5.4.4 ya Katiba kwamba mwanachama yeyote hatachukuliwa hatua za kinidhamu ama kuonywa ama kuachishwa ama kufukuzwa uanachama bila kujulishwa makosa yake kwa maandishi na kutakiwa kutoa majibu katika muda usiopungua wiki mbili.”

 Alitaja vipengele vingine ni kupewa nafasi ya kujitetea mbele ya kikao kinachohusika na atajulishwa kwa maandishi uamuzi wa kikao ndani ya wiki mbili baada ya kusikilizwa.

 Katika hatua nyingine, Kimesera alisema Chadema imepeleka majibu baada ya Mwigamba kupeleka barua yenye malalamiko kwa Msajili wa Vyama vya Siasa dhidi ya uongozi wa chama hicho.

Katika malalamiko yake, Mwigamba anadai kuwa katiba ya Chadema ilivurugwa na viongozi wa chama kwa kuondoa kinyume cha taratibu maelezo ya kifungu cha katiba ya chama yaliyokuwa yakiainisha ukomo wa vipindi viwili vya uongozi.

 Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Jaji Francis Mutungi, alithibitisha kupokea barua hiyo ya Mwigamba na kusema ofisi yake inaifanyia kazi.

 Kimesera jana aliliambia NIPASHE kuwa walipeleka majibu dhidi ya malalamiko ya Mwigamba baada ya kuagizwa na msajili kufanya hivyo kabla ya Desemba 19, mwaka huu.

 Katika barua yake, Mwigamba amemuomba msajili kutoa mwongozo kuhusu anachodai kuwa ni mgogoro wa kikatiba uliopo ndani ya Chadema kufuatia kipengele cha katiba kinachogusia ukomo wa uongozi kubadilishwa kinyume cha utaratibu.

 Novemba 22, mwaka huu, CC iliwavua madaraka viongozi hao na kuwataka wajieleze kwa maandishi ndani ya siku 14 baada ya kudaiwa kuhujumu chama kwa kuandika waraka wa siri unaodaiwa pamoja na mambo mengine, kuwadhalilisha viongozi wakuu wa Chadema.
 



CHANZO: NIPASHE

Read More »

BINTI WA MIAKA 17 ANASWA AKIJIUZA KATIKA GESTI BUBU


KIKOSI kazi cha Oparesheni Fichua Maovu ‘OFM’ Kanda ya Ziwa, kinaendelea kufukua uchafu unaofanyika jijini hapa, safari hii kimemnasa binti mwenye umri chini ya miaka 18 akifanya ukahaba wikiendi iliyopita bila wasiwasi wowote.
Anitha baada ya kunasa katika mtego wa OFM.
OFM Kanda ya Ziwa, kikiwa ni kitengo kipya kilichoteuliwa rasmi kushughulikia kadhia za mikoa yote inayozunguka Ziwa Victoria kilinasa tukio hili laivu na kulifuatilia kwa kina ili kutoa ukweli kamili kwa jamii.
HABARI KAMILI
Timu yetu ilishuhudia binti huyo akiwa amechanganyikana na mabinti wengine wakubwa wakijiuza kwa wateja wa baa mbalimbali katika eneo la Mabatini jijini hapa huku wakitumia gesti bubu iliyopo maeneo hayo.
Kwa siku tatu mfululizo, mapapazari wetu walimfuatilia na kujionea namna binti huyo mdogo akichukuliwa na mababa watu wazima na kwenda kula nao uroda kwa nyakati tofauti.
Anitha akivaa nguo zake baada ya kunaswa akifanya ukahaba.
AINGIA MTEGONI
Ili kupata ushahidi wa tukio hilo, makamanda wetu waliingia mzigoni na mmoja wao akajifanya mteja ambapo alimtokea binti hiyo ambaye alikubali kwenda kulala naye  kwa dau la shilingi 5,000.
Binti huyo aliyejitambulisha kwa jina la Anitha aliongozana na kamanda wetu hadi ndani ya gesti bubu inayotumika kwa uchafu huo bila kujua kwamba alikuwa ameingia ‘choo cha kiume’.
Anitha akiohojiwa baada ya kunaswa akiwa kazini.
OFM KAZINI
OFM wakiwa na wadau wengine waliokubali kushiriki katika zoezi hilo ambalo ni aibu kwa uongozi wa jiji hili na serikali kwa jumla, walikuwa tayaritayari jirani na gesti  hiyo wakisubiri maelekezo kutoka kwa kamanda aliyeingia na changudoa huyo mtoto.
Vifaa vya mawasiliano vya OFM vilifanya kazi yake vyema ambapo kamanda aliyekuwa chumbani alitoa maelekezo kwa wenzake kuwa changudoa yule, alikuwa amesaula ndipo wakaingia na kufotoa picha za kutosha.
MSIKIE MWENYEWE
Alipogundua kuwa kumbe ulikuwa mtego wa kumnasa aliomba asamehewe kwa madai kwamba alilazimika kufanya vile kwa lengo la kujitafutia maisha kwa vile kwao hali ni mbaya.
Anitha akiwa mikononi mwa wanausalama.
“Jamani mimi ni mdogo, nina miaka 17, sina baba wala mama na hali ya maisha ni ngumu ndiyo maana niliamua kuingia kwenye biashara hii,” alisema Anitha.
Hata hivyo, uchunguzi wa Risasi Mchanganyiko, umeonyesha kuwa, Anitha ni muongo kwani ametoroka nyumbani kwao Mahina, Nyakato ambako alikuwa akiishi na wazazi wake na kukatisha masomo yake akiwa kidato cha pili.
Chumba alipokutwa Anitha kitandani pakiwa na kinga.



WAZAZI SOMENI HAPA
OFM inatoa wito kwa wazazi kuwa makini na malezi ya watoto wao kwa kuwafuatilia mara kwa mara ili wasiharibike na kuiga tabia kama ya Anitha. Aidha, wazazi wa Anitha wanapaswa kuchukua hatua za makusudi kumwondoa binti yao katika biashara hiyo mbaya inayohatarisha usalama wa afya yake.

Read More »

MAMA SHARO MILIONEA AMTOA MACHOZI ICH MAVOKO


STORI kuhusu maisha ya mama mzazi wa staa wa komedi Bongo, marehemu Husein Mkiety ‘Sharo Milionea’, baada ya kifo cha mwanaye huyo imemliza Rich Mavoko ambaye alikwenda kumtembelea nyumbani kwake kijijini Lusanga, Muheza mkoani Tanga.
Rich Mavoko akifuta machozi alipomtembelea Mama Sharo Milionea.
Akiteta machache na Risasi Vibes, Mavoko alisema, yeye kama msanii aliguswa kwenda kumsalimia mama Sharo kwa kuwa wote ni wasanii na aliona mama huyo anahitaji faraja kutoka kwa watu waliokuwa karibu na mwanaye.
“Mama alifurahi sana kuniona. Tulizungumza mengi lakini niliguswa sana na matatizo aliyonayo mama yetu. Mama anasema, mali nyingi za marehemu mwanaye, amekuwa akizisikia tu lakini hajapewa.
Mavoko na Mama Sharo wakiwa katika kaburi la Marehemu Sharo Milionea.
“Kiukweli mama Sharo anatia huruma sana kwani faraja imepotea, mali za mwanaye hazioni, amebaki akitia huruma.
Unajua marehemu alikuwa akimsadia sana mama yake, ndiyo lilikuwa tegemeo lake kubwa. Ameondoka na kumuacha akiwa hana la kufanya, mbaya zaidi hata mali zake ambazo zingepaswa kumsaidia kipindi hiki, wajanja wamezidhulumu.
“Dunia haina usawa kabisa. Kiukweli inatia huruma sana. Nawasihi wasanii wenzangu na wadau wa sanaa, inatakiwa tukumbuke wenzetu waliotangulia tena kwa kuwaenzi kwa kila njia.
Marehemu Sharo Milionea enzi za uhai wake.



Kuna vitu vinauma sana amenieleza tangu kifo cha mwanaye haki zake nyingi hajui zilipo. Tuungane wasanii tuwasaidie wazazi wa wasanii wanaotangulia mbele za haki,” alisema Mavoko.

Read More »

MZEE WA KANISA ALIFUNGA KANISA! HUKO MBEYA


WAUMINI wa Kanisa la Nyumba ya maombi (House of Prayer Shield of Faith Christian Fellowship) lililopo jijini Mbeya wamekosa sehemu ya kufanyia ibada baada ya Kanisa lao kufungwa na mzee wa Kanisa hilo, Laurence Malongo.
Kanisa lililofungwa.
Mchungaji wa Kanisa hilo, Owden Mwakifuna amesema hivi karibuni mzee Mwalongo alifika kanisani na kuwataka waumini wote kutoka huku akionekana kutawaliwa na jazba.
Mchungaji Mwakifuna alisema kanisa hilo lilijengwa baada ya Malongo kutoa uwanja kwa ajili ya ujenzi wa kanisa hilo kama shukrani baada ya kufanyiwa maombi yeye na mwanawe na kupona magonjwa yaliyokuwa yakiwasumbua.
Viongozi wa kanisa wakiwa nje baada ya kanisa kufungwa.
Baada ya kanisa hilo kufungwa Mchungaji Mwakifuna alitoa taarifa kwa kiongozi wa kanda ya Mbeya, Mchungaji Isaya Laiser na kufanya vikao vya mara kwa mara ili kutatua mgogoro huo bila mafanikio.
Kufungwa kwa kanisa hilo lililopo kata ya Itezi kumewafanya waumini kutembea kilometa 10 hadi makao makuu ya kanda eneo la Pambogo Kata ya Iyela jijini Mbeya.
Ofisa Mtendaji wa Kata akihakiki viti.
Baada ya kufungwa kwa kanisa hilo, viongozi wa waumini hao waliandikia barua uongozi wa kata ambao uliitisha kikao Desemba 5 mwaka huu.
Kikao hicho chini ya Diwani wa Kata ya Itezi, Frank Mayemba ambaye alisema kiwanja hicho ni mali ya Malongo na hati yake haijabadilishwa.



Kikao kilimalizika kwa Malongo kuchukua viti 60 na kulifunga jengo hilo mbele ya uongozi wa kata ya Itezi na kuamriwa maandishi ya kanisa hili yafutwe kwenye kuta za jengo hilo mara moja.

Read More »

KIFO CHA KIGOGO WA CCM MWANZA, MAZITO YAIBULIWA


MAMBO mazito yameibuka baada ya kifo cha kigogo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Diwani wa Kata  ya Kisesa, Clement Mabina jijini Mwanza  kwa mwanasiasa mmoja kutajwa kuhusika na mauaji hayo, Risasi Mchanganyiko limeambiwa.
Clement Mabina enzi za uhai wake.
Habari zilizosambaa jijini hapa zinadai kwamba  mwanasiasa huyo (jina kapuni) andaiwa kuwagawia fedha baadhi ya wanakijiji waliohusika ili  kukatisha uhai wa Mabina.
“Hakuna asiyejua kwamba jambo hili lina mkono wa kisiasa ndani yake, mapema kabla ya marehemu kwenda Kanyama kwenye eneo la tukio mmoja wa wanasiasa mashuhuri alipita na kuwashawishi wanakijiji wasikubaliane na hoja zake na ikiwezekana wammalize,” alisema mmoja wa watu waliokuwa wakizungumzia kifo cha Mabina.
Mwili wa Mabina baada ya kushambuliwa.
Hata hivyo, polisi wanawashikilia watu saba wanaodaiwa kuhusika na mauaji hayo ya kinyama.
Kamanda wa Polisi wa Mwanza, Kamishna Msaidizi Mwandamizi, SACP, Valentino Mulowola, akizungumza na mwandishi wetu kwa njia ya simu, alisema hadi sasa watu saba wanashikiliwa na jeshi hilo.
Kamanda alisema watuhumiwa hao walikamatwa kwa nyakati tofauti jana ambapo jeshi hilo linaendelea kuwatafuta watuhumiwa wengine wanaodaiwa kuhusika katika mauaji ya  diwani huyo ambaye zamani alikuwa ni mwenyekiti CCM Mkoa wa Mwanza.
Katika tukio hilo la mauaji, Mabina aliuawa kwa kukatwa mapanga na kupigwa mawe ambapo alikutwa na majereha makubwa kichwani sehemu za kisogoni.
Kabla ya kuawa na wananchi  hao, marehemu alimpiga risasi mtoto Temeli Malemi (11) kwa  bahati mbaya wakati akijihami na mashambulizi ya wananchi hao.
Imeelezwa na Kamanda wa Polisi SACP Mulowola kuwa marehemu alikutwa na silaha mbili aina ya Short-gun na bastola moja.
Hata hivyo ndugu wa marehemu walishindwa kutoa ushirikiano kwa waandishi wa habari kuhusiana na habari zilizoandikwa na mitandao ya kijamii kuhusisha kifo cha ndugu yao (Mabina) na masuala ya kisiasa.



Aidha habari kutoka eneo la tukio zainadai kuwa mmoja wa watuhumiwa alikamatwa na simu ya mkononi ya marehemu,hata hivyo kamanda hakutaka kutaja majina  ya watuhumiwa hao kuhofia kuvuruga upelelezi.

Read More »

RAGE ALIA NA WALIOMUUZA OKWI YANGA


MWENYEKITI aliyesimamishwa wa Simba, Ismail Rage, amefanya kikao na baadhi ya wanachama wa timu hiyo na kutoa siri kwamba waliomuuza mshambuliaji Emmanuel Okwi kwa Yanga ni Waganda, SC Villa, lakini akasisitiza ni hujuma kutoka ndani ya klabu hiyo.
Emmanuel Okwi.
Championi Jumatano lilikuwa likipata ‘live’ kila kinachoendelea ndani ya kikao hicho kilichofanyika makao makuu ya klabu ya Simba, barabara ya Msimbazi jijini Dar es Salaam, jana.
Akionyesha mwenye masikitiko, Rage alisema kuna baadhi ya viongozi wa klabu hiyo wanahusika katika usajili wa Okwi aliyetua Yanga kwa mkataba wa miaka miwili na nusu.
Mwenyekiti wa Simba, Ismail Rage.
Rage, amesema Okwi raia wa Uganda, mpaka sasa anakabiliwa na kesi tatu muhimu na kuzitaja ya kwanza ni ile ya nyota huyo kukakabiliwa na mashtaka ya kutoroka katika klabu yake ya zamani ya Etoile du Sahel ya Tunisia (ESS).
Shitaka la pili ni kuhusu SC Villa, ambao walipewa Okwi kwa mkopo lakini wakamuuza Yanga na tatu ni kesi yake aliyoifungua Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa) kuhusu ESS, ambapo kabla ya shirikisho hilo kutoa majibu nyota huyo kukubali, Mganda huyo kauzwa Yanga.
“Nilipiga simu Fifa kutaka kujua kujua kuhusu Okwi, nikaambiwa kuna fedha dola 5,900 ambazo ni kwa ajili ya kusikilizwa kwa kesi yetu, mwisho ilikuwa saa nne asubuhi leo (jana). Barua ilishatumwa tangu Desemba 6, lakini hakuna aliyeijibu na wakaificha,” alisema Rage akitaka kudondosha chozi ‘live’.
“Saa tatu asubuhi nikatuma fedha hizo ambazo zitatoa nafasi ya kusikilizwa kwa jambo hilo. Kama ningechelewa, basi Okwi angeweza kuwa mchezaji huru kwenda Yanga,” alisema Rage katika kikao hicho kilichofanyika kuanzia saa 10:15 hadi saa 11:45 jioni.
Aidha, Rage amesema anajua kuwa kamati ya utendaji ya timu hiyo inachangia kumhujumu ili aonekane hafai katika klabu hiyo, ambapo sasa ataitisha mkutano mkuu Januari mwakani.
“Simba imejaa wanafiki, wanafanya mpango wachezaji waende Yanga. Mfano, Okwi alishatangaza anaitaka Simba, vipi hawakumsajili na utaona mambo yanaharibika kila nikiwa nje ya nchi. Pia TFF kuna watu kama hao na wanachangia kutuhujumu na kuniharibia,” alisema.
Kuhusiana na suala la uchaguzi, Rage rasmi ametangaza kwamba hatagombea nafasi hiyo tena na badala yake kuna mtu amemuandaa.
“Tayari nimemuandaa mtu, siwezi kumtaja sasa ila nitawaacha wanachama waamue utakapofika uchaguzi,” alisema Rage.
Mzigo wa Okwi umekuwa ukimuangukia Rage kwa kuwa ndiye alifunga safari kwenda kumuuza Tunisia, lakini akarejea mikono mitupu na dola 300,000 za mauzo zikabaki Tunisia na hadi leo ni hadithi.

    Read More »

    Join Swahili One Community, "Like" and you will be one of us forever

    Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...
    Copyright © 2013. swahili one Blog - All Rights Reserved
    Customized by: Grace Tommy The One | Powered by: BS
    Designed by: Creative Blogger