"BIFU" la Uwoya kuibiwa Mume na Lucy Komba ni Kutokana na Movie hii" Kwanini Nisimuoe" Angalia Picha Humu.

-->

Na Imelda Mtema
LILE sakata la staa wa filamu za Kibongo, Irene Pancras Uwoya kutuhumu kumshika ugoni staa mwenzake aliyemtoa kwenye gemu, Lucy Francis Komba limeingia sura nyingine kuafutia picha za filamu inayodaiwa kuchezwa na wawili hao kunaswa na Ijumaa, twende hatua kwa hatua.
Katika baadhi ya matoleo ya Magazeti ya Global Publishers zilichapishwa habari za mastaa hao kuzua bifu zito kufuatia Lucy kumchukua mwanasoka wa Rwanda ambaye ni mume wa ndoa wa Uwoya, Hamad Ndikumana ‘Kataut’ na kucheza naye filamu jambo ambalo Uwoya alilipinga.
KWA NINI UWOYA ALIPINGA?
Uwoya alipinga mumewe kushiriki filamu hiyo kwa sababu aliambiwa washiriki ni wawili tu, mumewe Ndikumana na Lucy. Filamu inaitwa Kwa nini Nisimuoe?
Kwa mujibu wa Uwoya, hajawahi kuona filamu ya kawaida inachezwa na watu wawili tu, akasema Lucy alitumia nafasi hiyo kuwa na mumewe kimapenzi.
Hata hivyo, Uwoya alisema akiviona vipande vya picha za filamu hiyo atajua ukweli.
Wiki iliyopita aliviona vipande hivyo na kuweka msimamo wake kwamba hakuna filamu ni mapenzi tu.
IJUMAA LAFUKUNYUA, LAIBUKA NA PICHA
Kama kawaida ya Magazeti ya Global Publishers, liwe Ijumaa, Uwazi, Ijumaa Wikienda, Amani, Championi au Risasi ni kuchimba mambo kwa undani na kuupata ukweli wa jambo, hivyo timu ya wanahabari wetu ilizama mitaani na kuzisaka picha za filamu hiyo.
Julai 23, 2013, Ijumaa lilifanikiwa kuzipata picha hizo ambazo moja baada ya nyingine zinawaonesha Lucy na Ndikumana wakiwa katika mapozi mbalimbali ndani ya filamu (angalia picha).
MWANZO, MWISHO NI WAWILI TU!
Katika picha hizo ambazo ziko mikononi mwa dawati la Ijumaa, wasanii walioonekana ni Lucy na Ndikumana tu hivyo kushibisha yale maswali ya Uwoya kuwa ni kwa nini filamu nzima ichezwe na watu wawili tu?
HADITHI YA FILAMU YADAIWA NI KISA CHA KWELI CHA UWOYA NA NDIKU
Habari za hivi karibuni zilisema kuwa,   cha ajabu, kisa kinachosimuliwa katika filamu hiyo ni cha kweli.
Ilidaiwa kuwa kisa hicho kilimpata Ndiku baada ya kukutana na Uwoya kwa mara ya kwanza kabla ya kufunga ndoa.
Madai hayo yanaongeza chachu katika moyo wa Uwoya na kuzidi kuamini kuna kitu kinaendelea kati ya mumewe na Lucy.
UWOYA AKATISHA ZIARA SWAZILAND
Uwoya alipotafutwa na Ijumaa juzi ili kumsikia msimamo wake kuhusu hali tete katika ndoa yake baada ya hisia zake kuwa anaibiwa mumewe na Lucy, alisema atapasua jipu atakapotua Bongo akitokea nchini Swaziland ambako alikwenda kwa ziara binafsi.
Alisema kuwa amelazimika kukatisha ziara na kurudi Tanzania kwa vile suala la Lucy na mumewe linamnyima raha kuendelea kuwepo ugenini.
“Narudi Bongo Jumatano (juzi). Unajua hili suala limeninyima raha kabisa. Siwezi kuendelea kuwepo huku ugenini. Nikifika nitatoa la moyoni,” alisema Uwoya.
 
LUCY AZUNGUMZA KUTOKEA DENMARK
Wakati Uwoya akizungumza kutokea jijini Mbabane, Swaziland, Lucy yeye alitoa sauti yake akiwa nchini Denmark kwenye Jiji la Copenhagen.
Alipoulizwa kuhusu tambo za Uwoya baada ya yeye kucheza filamu na mumewe Ndikumana, alijibu:
“Mimi sina cha kusema, yeye anajua mimi ni nani katika filamu. Mumewe kaonesha mapenzi ye kucheza filamu yangu, sasa anaposema ningemtaarifu yeye kama nacheza filamu na mumewe ili iweje? Kwa nini asimlaumu mume wake ambaye ndiye alipaswa kumtaarifu?” alisema Lucy.
Lucy aliongeza: Kama Ndiku angekuwa mtoto chini ya miaka kumi na nane nataka kucheza naye filamu hapo kweli, ningepaswa kumtaarifu Uwoya kama mama mtu, lakini mume, si sahihi kunilaumu.
MADAI YA HADITHI YA FILAMU KUWA KISA CHA KWELI
Kuhusu madai kwamba hadithi ya kwenye filamu hiyo ni kisa cha kweli kati ya Uwoya na Ndiku, Lucy alijibu:
“Teh! Teh! Si kweli bwana. Kama Uwoya ndiyo kasema hivyo basi ana kisa kinachofanana na cha filamu yangu. Mimi filamu ni yangu na hadithi ni yangu.”
WAONGOZA FILAMU BONGO WANASEMAJE KUHUSU WATU WAWILI TU?
Ili kujifunza juu ya wasanii wawili kucheza filamu nzima, Ijumaa liliwatafuta baadhi ya waongoza filamu Bongo.
Jumanne Kihangala ‘Mr Chuz’: Kusema kweli ni vigumu sana. Labda kama zile filamu za porini, mtu anakimbizwa na wanyama (documentary).
“Lakini kucheza filamu za mjini halafu wawili tu, mnagombana wenyewe mnapatana wenyewe ni kazi sana,” alisema Chuz.
Jacob Steven ‘JB’: Du! Labda kama utakuwa umekusudia kupunguza bajeti, lakini pia haitakuwa filamu nzuri, wawili tu?! Kwanza ni filamu gani hiyo ya watu wawili tu?
Ijumaa lilimkatia simu.
Mahsin Awadh ‘Dk Cheni’: Mh! Zipo kama mtu mwenyewe atakuwa ameamua, lakini sidhani kama sokoni itakubalika. Ni nani huyo kwani?
Ijumaa likamkatia simu.
Wazoefu wengi wa filamu walisema documentary ndizo zinaweza kuwa na watu wawili lakini si filamu.


source: GPL

Read More »

Kumekucha "BONGO MOVIE", Nisha naye Akimbia na Samani za Ndani za Rafiki yake.

-->



Na Gladness Mallya
MSANII wa filamu za Kibongo, Salma Jabu ‘Nisha’ ametupiwa tuhuma nzito za utapeli wa samani za ndani baada ya kupewa hifadhi na shoga’ke aitwaye Amina Mrisho anayeishi Ilala jijini Dar, Ijumaa limetonywa.
Salma Jabu ‘Nisha’.
Kwa mujibu wa Amina, tukio hilo limetokea mwaka 2011 baada ya msanii huyo kukosa fedha za kulipia kodi na kuomba hifadhi kwake.
“Alitakiwa kuondoka katika nyumba aliyopanga akaomba hifadhi kwangu nikamsitiri kwa kuwa alikuwa ni rafiki yangu, akahamia na vitu vyake vyote vya ndani,” Amina alianza kushusha madai hayo na kuendelea:
“Baada ya muda alitangaza kuziuza samani zake kwa shilingi 750, 000 ili apate fedha za kuendeshea maisha, nikaahidi kuzinunua na nikamtangulizia shilingi 500,000 kama malipo ya sofa, meza ya runinga, dressing table na meza ya jikoni.”
Hata hivyo, msichana huyo alisema kwamba kabla mwezi haujaisha, Nisha alibadilika na kutaka fedha zilizobaki kwa nguvu huku akimpa vitisho kwa kumwambia kuwa atamkomesha kwa kuwa risiti zote za samani hizo alikuwa nazo.
Amina Mrisho.
Inazidi kudaiwa kwamba Nisha alienda kutoa taarifa polisi na kudai kwamba Amina alimwibia samani zake.
“Pamoja na kujieleza polisi muafaka ulifikiwa kwamba Nisha achukue samani zake na miye sikuambulia chochote,” alisema Amina.
Baada ya malalamiko hayo, paparazi wetu alimtafuta Nisha ili kupata ukweli, naye alikuwa na haya ya kusema:
“Kwanza huyo Amina simfahamu na katika maisha yangu sijawahi kukaa kwa mtu kwa sababu ya kuishiwa hela ya kulipia kodi. Mama yangu ana nyumba kubwa tu, ningewezaje kuiacha na kwenda kukaa kwa mtu baki?”
“Ukishafanikiwa lazima kuna watu wataibuka na kusema maneno mabaya ili wakushushe kama huyu miye wala simfahamu ni muongo tu.”


SOURCE: GPL

Read More »

"UFUSKAA" Angalia Madanguro yalivyogunduliwa, Wanawake wanajiuza Hadharani.


Na Chande Abdallah
ILE Oparesheni Fichua Maovu ‘OFM’ chini ya Global Publishers ipo kazini! Safari hii imekutana na tukio la aina yake baada ya kumnasa kikongwe mmoja anayedaiwa kumiliki idadi kubwa ya madanguro katika uwanja wake na kuwapangisha makahaba katika eneo maarufu kwa jina la Kijiji cha Makahaba.

Awali kachero wa OFM alipokea ujumbe mfupi ulioelezea ufuska unaofanywa na mabinti ambao hupewa eneo na kujenga vibanda kisha kujiuza kwa bei chee katika kijiji hicho maeneo ya Kigamboni jijini Dar.
Mzee Matutu ambaye ni mmiliki wa eneo linalofanyiwa ufuska.
Uchunguzi wa gazeti hili ulibaini kwamba, eneo hilo linalofanyiwa ufuska huo linamilikiwa na kikongwe aliyejitambulisha kwa jina la mzee Matutu akidaiwa kuendesha maisha kwa biashara hiyo ya madanguro.
Baada ya kujiridhisha na uchunguzi kuwa ni kweli jambo hilo linafanyika eneo hilo, OFM ililivamia ikiwa na mjumbe wa mtaa huo aliyefahamika kwa jina la Abbas na kujionea madanguro yaliyojengwa kwa mstari ambapo milango yake iliachwa wazi huku ndani wakionekana mabinti wakiwa wamejilaza kihasarahasara wakiwatega wateja wanaopita katika mtaa huo.
Madanguro hayo ambayo kwa hesabu ni takriban kumi na nane, yamejengwa kwa aina yake ambapo mengi kati ya hayo yana ukubwa wa kutosha kuingia kitanda kidogo pekee.
Baada ya kujionea hayo, kikosi kazi sambamba na mjumbe huyo kilimtafuta mzee Matutu na kufanikiwa kuzungumza naye kuhusu madanguro hayo na namna anavyoyaendesha ambapo alikiri kuwa yeye ni mmiliki wa eneo hilo na huwa anapokea shilingi 30,000 kwa mwezi kwa kila mwanamke na fedha hiyo ndiyo inayomsaidia kuendesha maisha.
“Sina kazi nyingine ya kuniingizia kipato zaidi ya hii ya wasichana licha ya kwamba sijawaruhusu wafanye biashara hiyo. Fedha hiyo ndiyo inanisaidia kwa mahitaji yangu,” alisema kwa tabu mzee Matutu huku akimtaja msimamizi wa madanguro hayo kuwa ni mpwa wake.
Kwa upande wake mjumbe wa mtaa huo, Kassim alisema kuwa serikali ya mtaa imejitahidi kwa kadiri ilivyoweza kuwaondoa mabinti hao lakini wamekuwa wakirudi kila mara.
Alipoulizwa hatua waliyoichukua kwa mmiliki wa madanguro hayo ambaye ni mzee Matutu, kiongozi huyo alibakia kusikitika asijue hatua gani ya kumchukulia mzee huyo ambaye hata wakimpeleka kwenye vyombo vya sheria anahisi itakuwa ni uonevu kwa kuwa hana msaada mwingine wa kifedha zaidi ya fedha kutoka kwa mabinti hao.

 SOURCE: GPL

Read More »

Mke anayedaiwa kupanga kumuua mumewe kortini



Arusha. Mwanamke anayedaiwa kupanga njama za kumuua mumewe wa ndoa na mtoto wa mume huyo, amepandishwa mahakamani akiwa na mtuhumiwa mwingine wa mauaji hayo.
Janeth Jackson (32), mkazi wa Moshono, Arusha na Novatus Elias, walifikishwa jana mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Arusha /Arumeru, Devotha Kamuzora, wakisomewa makosa mawili ya kula njama ya kutaka kumuua Simon Jackson ambaye ndiye mume wa Janeth.
Mwendesha Mashtaka wa Serikali, Edna Kasala, alidai mahakamani hapo kuwa washtakiwa wote walitenda kosa la pili la kula njama na kutaka kumuua Desderi Sabas, ambaye ni mtoto wa mke mwingine kwa mume huyo anayeishi Bukoba, mkoani Kagera.

Washtakiwa wote hawakutakiwa kujibu lolote kwa sababu Mahakama hiyo kisheria haina mamlaka ya kusikiliza kesi za mauaji.
Kasala iliomba mahakama kuwanyima dhamana washtakiwa, kwa sababu watuhumiwa wengine wawili wanatafutwa hivyo na upelelezi haujakamilika.
Alidai kutokana na uzito wa tuhuma hizo, maombi hayo ya kuwanyima dhamana washtakiwa yameambatana na hati ya kiapo ya Mkuu wa Upelelezi Makosa ya Jinai Mkoa wa Arusha.
“Mheshimiwa tunafahamu kwamba dhamana ni haki ya washtakiwa kikatiba, lakini kutokana na mazingira ya kesi hii kuwa magumu, tunaomba dhamana isitolewe ili kuwatafuta watuhumiwa wengine wa kesi hii,” alidai Kasala.

Kwa upande wake,Wakili wa utetezi, Fidelis Peter, alipinga maombi hayo na kutaka mahakama itoe dhamana kwa washtakiwa kwa sababu ni haki yao ya kikatiba na kwamba hilo ni kosa lao la kwanza.
Sababu nyingine ya kupinga maombi ya upande wa mashtaka, ni kwamba washtakiwa wanaweza kuvuruga upepelezi wakiachiwa siyo za msingi kwani ni watu wanaoaminika katika jamii.
“Mheshimiwa sababu za kuwanyima dhamana washtakiwa hazina uzito wowote, pia mshtakiwa wa kwanza (Janeth) ana mtoto wa miezi sita na tangu akamatwe alhamisi iliyopita hajamwona wala kumnyonyesha hivyo anastahili kupewa dhamana,”alidai Wakili Peter.

Hata hivyo, baada ya kusikiliza maombi ya pande zote mbili, Hakimu Kamuzora, alikubaliana na maombi ya upande wa mashtaka na kuamuru watuhumiwa wapelekwe mahabusu hadi Agosti 5, mwaka huu kesi hiyo itakapotajwa tena.

Katika kesi hiyo iliyovuta hisia za watu wengi jijini hapa, inadaiwa Janeth alitaka kumuua mumewe ambaye ni mfanyabiashara wa madini ya Tanzanite na mwanaye wa kiume, ili arithi mali na utajiri aliona.

SOURCE: MWANANCHI

Read More »

Atakaethubutu Kiugusa Tanzania Kukiona cha Moto - Kikwete


Rais Jakaya Kikwete ametuma ujumbe kwa wale wanaoitishia Tanzania. Amewaambia wakithubutu watakiona cha mtemakuni kama ilivyokuwa kwa Idd Amin wa Uganda.
Alisema mamlaka za ulinzi na usalama zilimdhibiti Amin alipofanya uvamizi katika ardhi ya Tanzania mwaka 1978 na kwamba hazitashindwa kufanya hivyo kwa mtu mwingine yeyote atakayechezea usalama wa nchi.
Wakati Rais akisema hayo, Mkuu wa Majeshi, Jenerali Davis Mwamunyange amewahakikishia wananchi kuwa wakati wote jeshi liko imara na kuwataka wasiogope lolote.
Viongozi hao walisema hayo jana katika maadhimisho ya Siku ya Mashujaa iliyofanyika katika Kambi ya Jeshi ya Kaboya iliyopo Muleba, Kagera.
“Sihitaji kusema tena, mmeshamsikia Mkuu wa Majeshi, atakayejaribu atakiona cha mtemakuni, laleni usingizi na msiwe na wasiwasi, msisikilize maneno ya mitaani,” alisema Rais Kikwete na kuongeza:
“Wakati wowote, saa yoyote tuko tayari kulinda nchi yetu. Hatuko tayari kuona amani inaharibika nchini, hatuwezi kuruhusu mtu yeyote kuimega au kuichezea nchi yetu kama alivyofanya Idd Amin.”
Katika siku za karibuni kumekuwa na kauli kadhaa kutoka kwa baadhi ya viongozi wa nchi jirani ambazo zinatafsiriwa na wananchi kwamba ni za kuitisha Tanzania.
Jenerali Mwamunyange alisema jeshi wakati wote liko imara kuwalinda wananchi na nchi kwa jumla hivyo wasiogope...“Endeleeni na shughuli zenu na msiogope mtu yeyote, fanyeni kazi zenu bila wasiwasi.”
Huku akishangiliwa na mamia ya watu waliohudhuria maadhimisho hayo, Jenerali Mwamnyanye alisema yeyote atakayethubutu kuchezea usalama wa nchi atakiona cha mtema kuni.
Akizungumzia Siku ya Mashujaa, Rais Kikwete alisema ni siku ya kuwakumbuka mashujaa waliojitolea maisha yao wakati wa Vita ya Kagera kuilinda nchi yao ili iwe salama na yenye amani.
“Kuhakikisha usalama wa nchi kuna gharama yake kwani kuna wengine walikufa na wengine wakabaki na vilema kwa ajili ya hilo. Wale ambao wamebaki na wana matatizo lazima tuwaangalie vizuri na vile ambavyo havijafanyika tutavishughulikia kwani kutetea taifa ni kazi ngumu.”
Maadhimisho hayo yalihudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwamo, Makamu wa Rais, Dk Gharib Bilal, Rais wa Zanzibar, Dk Mohammed Shein, Jaji Mkuu wa Tanzania, Othman Chande na Jaji Mkuu wa Zanzibar, Omar Othman Makungu ambao wote walipewa nafasi ya kuwasalimia wananchi waliohudhuria maadhimisho hayo.

SOURCE: MWANANCHI

Read More »

Mwanaume Akatwa Miguu baada ya Kufumaniwa na Mke wa Mtu



Na Mwandishi Wetu, Kilosa
ALI Omar, mkazi wa Kijiji cha Mabana, wilayani Kilosa, Mkoa wa Morogoro anashikiliwa na polisi kwa kosa la kumkata miguu Said  Iddi kwa kumtuhumu kumfumania na mkewe aliyejulikana kwa jina la mama Ali, mkanda mzima upo mikononi mwa Amani.


Mke wa mtu sumu: Said  Iddi akiwa chini baada ya kukatwa miguu na Ali Omar.
Tukio hilo la kikatili lilijiri Julai 15, mwaka huu wakati Said na mama Ali walipokuwa ndani ya nyumba ya Ali iliyopo kijijini hapo.
MANENO YA SHUHUDA
Akizungumza na mwandishi wetu, shuhuda mmoja ambaye jina lake halikuweza kupatikana mara moja alisema Said alifumaniwa ndani ya nyumba asubuhi akiwa na mke wa Ali baada ya kuwekewa mtego ambao ulimnasa vizuri.
“Ali alipewa habari na kijana mmoja aitwaye God kwamba mkewe si mwaminifu katika ndoa, akamwongezea kuwa anatoka kimapenzi na Said. Ndipo Ali na mnyetishaji wake huyo walipopanga kumfumania jamaa,” alisema shuhuda.
Chini ya ulinzi: Mwenye mali, Ali Omar (kati) akiwa chini ya ulinzi baada ya kumkata Said.
Aliongeza kudai kuwa, Said ni msimamizi wa mashamba ya Ali kijijini hapo na kwamba God ni mtoto wa mwenye nyumba ambayo Ali amepanga kijijini hapo.
MPANGO WA FUMANIZI
Habari zinapasha kuwa mara baada ya mnyetishaji kutoa taarifa za usaliti huo, Ali alimtafuta  ‘baunsa’ ambaye jina lake halikuweza kujulikana mara moja na wakaweka mtego kwa kujificha karibu na nyumba hiyo ambayo Said angeingia ili kuivunja amri ya sita ya Mungu.
Umbea kazi: Kijana aitwaye God (kulia) aliyetoa taarifa kwa Ali naye akiwa chini ya ulinzi.
Katika kufanikisha mtego huo, mmbeya huyo alipewa jukumu la kuhakikisha nyendo za Said na mama Ali siku hiyo zinarekodiwa mpaka kuingia ndani ya nyumba hiyo na kumtaarifu Ali ambaye siku hiyo alimuaga mkewe kwamba amesafiri.

SAID ATINGA NYUMBANI KWA ALI
Habari zinasema mtoboa siri huyo alimwambia Said kuwa Ali amesafiri na ndipo jamaa akafunga safari kwenda kwa mama Ali kwa nia ya kujivinjari licha ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhani ukifikia katikati.
Mwanamke hutulii?: Mke wa Ali Omar naye akipelekwa polisi baada ya tukio hilo.
Habari zinadai mara baada ya kufika kwa Ali, Said aliingia ndani ya nyumba bila kujua kwamba mwenye mke alikuwa amejificha jirani akisubiri mtego unase.
Inasemekana Said akiwa ndani, Ali na baunsa wake waliibuka kwa kutaarifiwa na God na kumnasa jamaa huyo huku akidai ni mgoni wake. Alimuuliza maswali kadhaa, yakiwemo haya:
“Umekuja kufanya nini ndani ya nyumba yangu? Kwa nini umekaa na mke wangu?”
Habari zinasema Said alijibu hakuona ubaya kwa kuwa yeye ni mwangalizi wa mashamba ya mwanaume huyo hivyo anaweza kuingia ndani kwake wakati wowote.
Said  Iddi akiwa amezungukwa na wananchi baada ya kukatwa miguu.
MWENYE MKE ATIBUKA NA MAJIBU, AMWAGA DAMU
Jibu hilo lilidaiwa kumtibua Ali na ndipo yeye na baunsa wake wapomfunga kamba miguuni Said na kuanza kumkata kwa panga mguu mmoja kisha kuugeukia wa pili.
Said alipiga mayowe yaliyowafanya wanakijiji kukimbilia eneo la tukio kwa lengo la kujua kulikoni ambapo walimkuta Said akiwa anavuja damu na sehemu ya nyuma ya miguu ikiwa nyanga’nyang’a.
Said akipelekwa kwenye difenda.
MWENYE MKE AKIMBIA, ANASWA
Ali, God na baunsa walikimbia eneo hilo. Baadhi ya wanawake walitumia khanga zao kuifunga miguu ya Said kwa lengo la kujaribu kuzuia damu isiendelee kumwagika. Said alikuwa akilia sana.
“Wanakijiji walichukizwa sana na ukatili uliofanywa na Ali, hivyo wakaanza kumsaka na kumkamata kichakani akiwa amejificha pamoja na God. Alipewa mkong’oto kwa lengo la kutaka kumuua, lakini viongozi wa kijiji walisihi asiuawe bali afikishwe kwenye kituo cha polisi,” alisema shuhuda.
...Akiingizwa ndani ya difenda.
MKE, MUME, MMBEYA WAFIKISHWA POLISI
Polisi wa Kituo cha Dumila waliitwa na kumchukua Said, Ali na God kwa kutumia gari aina ya Land Rover lenye namba za usajili T 750 AAJ. Mke wa Ali yeye alipelekwa polisi kwa pikipiki.
Walipofika kituoni, Said alipewa fomu ya matibabu ya polisi (PF 3) na kupelekwa Hospitali ya Wilaya ya Kilosa kwa matibabu.
“Pale hospitali Said alishonwa miguu yote lakini madaktari wakaamua ahamishiwe katika Hospitali ya Mkoa wa Morogoro kwa matibabu zaidi,” alisema shuhuda huyo.
Bwana Said akiwa ndani ya difenda.
ANAWEZA ASITEMBEE TENA
Akaongeza: Daktari mmoja alisema haamini kama jamaa (Said) atatembea tena kwa sababu zana iliyotumika kumkata ilifika hadi kwenye mishipa ya nyuma ambayo ndiyo humfanya binadamu aweze kusimama na kutembea.
Said akishonwa katika Hospitali ya Wilaya ya Kilosa.
BAUNSA ASAKWA
Afisa mmoja wa polisi kituoni hapo ambaye hakupenda jina lake liandikwe gazetini kwa kuwa si msemaji, alisema wanaendelea kumsaka baunsa aliyeshirikiana na Ali kumkata miguu Said.
...Said akizidi kupatiwa huduma.




 SOURCE: GPL

Read More »

Angalia Mfanyakazi wa Subway alivyoweka "UUME" Wake katika Mkate wa Wateja, Kisha ku Post Picha Instagram, Afukuzwa kazi Mara Moja.


Kwa wale wapenzi wa kula Sandwich huko Marekani hili limewachefua saana, maana huyu jamaa sikui alikuwa anafikiria nini baada ya kuweka picha hizo chafu katika Instagram na video huku akijitambulisha" Mimi..... Leo ndo Muandaaji wako wa hii Sandwich"

Kampuni ya Subway ambayo jamaa huyo alikiuwa anafanya kazi wamemfukuza kazi mara moja jamaa huyo na kuwaomba radhi wateja wake kwa kitendo hicho kiovu cha mfanyakazi huyo.


Read More »

Mzigo wa Kodi kwa Wananchi haubebeki, Au vp Kipanya?!!!


Nadhani hili suala limekuwa dhahiri sasa, maana mzigo wa Kodi kwa Wananchi ndo unazidi huku wazee wa Mjengoni wakizidi kubuni Mizigo Mingine Kila leo huku hali ya Maisha ya Mtanzania ikizidi kudorora.

Read More »

Dereva Aliyesababisha Ajali Akamatwa, Angali Picha ya Gari Lake, Loh! Kumbe Hata Usukani Hana Badala yake Aendeshea Koleo!!


Polisi huko Australia wanamshikia Mtu mmoja baada ya kusababisha ajali akiwa na gari lake. Cha kustajaabisha zaidi ni pale polisi walipolikagua gari la mtuhumiwa huyo na ndipo walipokuta maajabu, kwani hakukuwa na Usukani ila ni Koleo.

Mtuhumiwa huyo alipelekwa katika vipimo maalumu vya madawa ya kulevya na Pombe, majibu yameonesha alikuwa katika athari ya madawa hayo wakati anaendesha, pia hana leseni na matairi ya gari lake yalikuwa yameisha kabisa.



Read More »

Angalia "MATUSI" ya Kanye West, Choo katika Nyumba Mpya Chagharimu Bilioni 1.2 za Ki Tanzania.


Haya sasa, Mambo yamebainika kuhusu shooping ya kuikarabati nyumba ambayo Kim na Kanye West Wameinunua. Katika jumba hilo la kifahari ambayo ndani yake kuna Fenicha za thamani ya hali juu mno, Miongoni ya fenicha hzo ni Choo chenye thamani ya Shilingi za Kitanzania Bilioni 1 na Milioni 200.

Sasa vuta picha ndugu yangu Mtanzania, kama choo tu Bilioni hizo jumba lenyewe litakuwaje? Bila kusahau Master Bedroom inagharimu Tsh Bilioni 1 na Milioni 650 za Ki Tanzania.

Kitchen bling: The couple are also said to be blinging out their kitchen with a Swarovski-encrusted fridge freezer and almost $1 million worth of Electrolux appliances
 Swarovski-encrusted fridge freezer, Ambalo lipo jikoni, pia jikoni pana gharimu zaid ya Bilion 1.6 za Tanzania

Beds fit for a king: Kanye has also reportedly splurged on six special-edition beds from the company which supplies London¿s Savoy Hotel, the total coming to $1 million
Chumba cha hadhi ya Kifalme, zaidi ya Bilioni 1.7 za Kitanzania zimedondoka humo

New home: The exterior of Kim and Kanye's new Bel Air home before renovations
Taswira ya Mbele, kabla ya Marekebisho

Before: A living room featured in the couple's new home which will no doubt be totally transformed
Taswira ya Ndani, kabla ya Marekebisho







Read More »

Nilifanya Mapenzi na Mama Yangu, Nikaua watoto 27, Nilikula Ndimi 100 ili nisikamatwe wala kuonekana na Polisi.


Kwa Raia wa Nigeria, Jina la Shina Rambo sio Geni Miongoni mwao, hii ni kutokana na jinsi Jangili huyo alivyowasumbua Raia na Vyombo vya Dola kwa zaiida ya Miaka 5 huju akifanya Uhalifu, Mauaji na Unyang'anyi wa kutumia Silaha Mchana Kweupe Bila Kukamatwa.
Shina Rambo


Fuatilia Kisa chake hapa:- Kwa Kiingereza

It was a beautiful Saturday morning, I was garbed in a pair of jeans, on a pair of Timberland boots, a military sweat shirt, and my JackMoody denim jacket. I had been attacked by men of the underworld the night before whilst we were on production, at the office. So I slung my black Ted Baker satchel across my right shoulder, armed with my camera, my midget, and some other small gizmos.

I was more determined, to embark on this adventure, than ever before. I was headed for the ancient city of brown roofs, Ibadan where a one-time Nigeria’s most notorious and dreaded bandit that ever lived SHINA RAMBO mounted the pulpit to preach!!! What an irony you would say.

Now Mathew Oluwanifemi, Shina Rambo was a name that sent shivers down the spine of people who lived in the South West of Nigeria and even outside Nigeria, like Benin Republic and neighborhood, in the 1990’s. 
He was a hardened criminal, a terror and killer, one whom men of the security agencies will never forget in a haste!

A man mountain, towering about 6ft 5inch, well built, dark skinned and sweltering eyes, he carried out his operations, like  a movie, in the broad day light, with sophisticated weapons, and bullet belts and explosives strapped roundabout him! He specialized in robbing exotic cars on highways and banks. Nothing could stop him, not even security operatives, he was totally invincible. He was Shina Rambo!

He was born in the year 1958 to a military man who was a bad egg in the service. His father was from Abeokuta in Ogun state, but his mother was a native of Sabongida–Ora in Edo state. His father had over 18 wives, as was the norm for soldiers to impregnate virtually every woman they met where they were posted to.

His father used his military influence to rob innocent citizens, and always brought huge amount of money home. This used to entice little Shina. He recalls, “I remembered when I was about 7 years old, my father came home with a lot of money, foreign currencies, with blood on it, and they were using something like a woman’s scarf to wipe it, then I asked him, is this an animal’s blood, or human blood?  But he wouldn’t answer me, they were just drinking, smoking, and merry making.”

Shina was already indoctrinated into the underworld by his father at a tender age of 7 without him knowing it, as he would sit in front of his son, to dismantle and assemble all sorts of weapons and then polishing them in preparation for an operation. This went on for so long till one day, little Shina, entered into his father’s room while he had stepped into the toilet, and saw a dismembered gun on the floor. He sat down in front of it, and bit by bit, he had assembled it effortlessly in no time at all. His father came out of the toilet, and saw his son, with a loaded gun in his hands. Shina flashed back and said, “That day my father was so disappointed, that he wanted to kill me, he grabbed the gun from my hand and shot straight at me, but I miraculously escaped out of the room.

Then he waited for me to be less alert at night he came to my room with a machete and tried to behead me, but once again, I escaped, but the machete caught my left leg. (rolled up his trouser to show us the large scar, that made everyone sighed in pity). It cut me so deep I thought I was never going to walk again.  That day I knew I had graduated, all that was left was to pull the trigger, and I was so eager.


Shina Rambo became so notorious in no time, and was hell bent on succeeding in his career as an armed robber, that he went through any length to secure spiritual powers for fortification. To the extent of pounding over 27 live new born babies in the mortar with a pestle, cutting off about 100 human tongues and cooking them to eat, visiting the spiritual river called river of life in Ogoja, Cross Rivers State, living in an Iroko tree for days, and sleeping in the cemetery.

He was given a spiritual wife who always followed him for any operation, she dressed like an Alhaja, people thought she was human, but she was a spirit, that was why they never saw her face.  He said she was his personal driver, that she could drive from Nigeria to Cotonou, in the speed of light. Hear him. ”I was involved in so many rituals, that I can’t start naming them now, I was so powerful, I went underground, inside trees that looked like a city, a lot of beautiful houses inside the tree, I had my own too, I went into a river called  River of life in Ogoja, where a lot of politicians and wealthy men used to come, I had several personalities, I could change my form whenever I wanted to, that’s why the police were busy killing innocent people, and thought they were killing Shina Rambo.

The 9 herbalists that gave me that power, I became stronger than them, one day I went to their shrines, and killed all of them, so that they don’t reveal my secrets. I had too many powers; my spiritual wife could drive any car in this world or out of it, no police vehicle, or anyone for that matter, could ever chase and catch me during an operation. She was out of this world, and when she had completed her operation, they took her away from me. I could give anything to get powers, and the elders knew, so they also gave me anything I wanted.

I once beheaded hundred men, and gave them the heads fresh, they were so happy with me that they made me invincible. No matter the kind of bullet you shot at me, it was just like pure water on my body. I could give anything to get power, but of all the things I did to get power, the one that still breaks my heart the most, is sleeping with my mother. My father is dead now, but my mother is still alive, and she lives with me she is 85 years old, whenever I set my eyes on her, I just start crying. I can`t bear it.

Shina Rambo was a raging terror, he was infallibly dangerous, the police dreaded him, both in Nigeria, and Benin Republic, his place of interest for business. He would go to police stations, in broad daylight and kill every policeman there, drive to check points and open fire on every policeman on duty, he didn’t like the police at all, and was never afraid of them, he operated in broad day light armed to the teeth looking like Johny Rambo, in the popular Sylvester Stalone movie, “First Blood”.

He once robbed 40 exotic cars in one day and drove all of them in a convoy, from Lagos to Cotonou, unstopped. He was powerful; he was wealthy, and impenetrable. He was a tin god, apparently belched from the very arroyo hell, we all dreaded him. He had a wife and three children, but he lost all of them in one day during a bloody police raid whilst he was away on operation. His wife was his stabilizing factor his life changed afterwards. He says “my wife was everything to me, I was forbidden by the elders to sleep with any other woman apart from her, I could gather about 50 women around me in a hotel, and they will just be playing with me, we would smoke, drink, and sniff cocaine, I will give them money but I will never sleep with them. I will go back home to my wife and sleep with her. That was why the police never caught me.

She knew my job, she knew what I was, I never left them alone at night, I operated in the day time and go back home to my family at night. I had everything, I was very wealthy, I once spent 50 million naira in a day.  I did it a lot, there was one day that we were coming from an operation and it seemed as if my powers were going to fail me, the police and the army were almost closing in on us, so we had to drive into a crowd and threw millions of naira in the air, there was commotion, everybody was busy picking naira notes even the police, until we escaped. I was too rich, but anything the devil gives you never lasts, he will collect more from you, it’s only the devil that will give you Fila, (cap) and ask for Iro and Buba.(wrapper and top). I lost everything, all the money, my family; I was so powerful the police couldn’t catch me but I lost it all.

I had to surrender myself to the police, and I was arrested and jailed for 11 years. When I was serving my jail term in Agodi prisons, Ibadan, Prophet T.O Obadare came visiting, and having been encouraged several times by the Christian brothers and sisters in the prison to give my life to Christ, he prayed for me and converted me, and changed my name to Oluwanifemi, and it was so miraculous, the next day I woke up and started speaking in tongues. It was during the time of President Olusegun Obasanjo, that we were granted freedom.

At this point, I was glued to my seat, the revival where Shina Rambo gave this exclusive confession was on an open ground revival in the ancient city of Ibadan, right in front of me, on stage, was Evangelist Mathew Oluwanifemi, the once feared Shina Rambo, clad in a loose fitting shirt, black pants and a pair of leather sandals with a black Holy Bible in his hands, gigantic dark skinned and bald headed, still had those fiery looks, and stealth movement.

I was more transfixed than focused, God is indeed awesome, he picked the offering basket  raised it to the congregation  prayed and asked who had anything to give to  God,  at first  I was reluctant, my mind was occupied and out of  an innate compulsion, sheer curiosity I stood up, dipped my hand in my pocket walked towards him briskly and calculatedly  brought out my offering, dropped it into the basket, and looked deep into his eyes, I had too many things to ask him, there were too many questions unanswered. He looked back at me, and spoke in Yoruba, saying God bless you my brother; we know your type when we see them.

The congregation broke into a mild giggle, as all eyes were on me as I went back to my seat, with a lot of things on my mind, and the red light on my midget still blinking, in the breast pocket of my jacket…..

Read More »

Aibuu "SHILOLE" Aiba Simu za "Daimond", Alipewa na Ndugu wa Daimond South Africa, Hajampa Mwenyewe Hadi Leo!!!!



Stori:Shakoor Jongo na Musa Mateja
STAA wa filamu na muziki wa Bongo Fleva, Zuwena Mohammed ‘Shilole’ ameingia matatani akidaiwa kuingia mitini na simu tatu za mkononi alizoaminiwa nchini Afrika ya Kusini alikokwenda kufanya shoo.
Mfano wa aina ya simu anazo daiwa kuiba Shilole
Msanii huyo alikumbwa na kasheshe hilo Julai 19, 2013 nyumbani kwa mwanamuziki wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’, Sinza Mori, Dar.
Siku hiyo Diamond alikuwa akifuturisha na aliwaalika watu mbalimbali wakiwemo mastaa lakini nusura futuru iingie doa kufuatia zogo hilo.
ISHU ILIKUWAJE?
Ndugu wa Diamond aitwaye Majaliwa Majuto ‘Q Boy’ alidai ndiye mwenye simu hizo. Alisema miezi kadhaa iliyopita, Shilole alikwenda nchini humo kufanya shoo ya muziki. Wakati wa kuondoka alimpa simu tatu, Ipad, Samsung Galaxy na Blackberry ili akifika Bongo ampe Diamond lakini msanii huyo hakufanya hivyo.
“Alikuja Sauzi kufanya shoo, wakati wa kuondoka nilimpa simu tatu amletee Diamond lakini nashangaa hakufanya hivyo na mimi tangu nirudi Bongo simpati, kila nikimpigia simu hapokei, leo ndiyo tumekutana hapa kwa Diamond,” alilalama Q Boy.
DIAMOND ALIAMBIWA SIMU ANAZO SHILOLE
Alisema awali akiwa nchini humo baada ya kumkabidhi mali hizo, alimpigia simu Diamond na kumtaarifu kuwa ‘mzigo’ anao Shilole, akashangaa staa huyo kujibu kwamba hajazipata wala hajamwona Shilole.

SHILOLE AJITETEA
Katikati ya mzozo huo, Shilole alijitetea kwa kusema: Mi namdai rafiki yake fedha yangu ya shoo iliyobaki, kama shilingi laki nane hivi ndiyo maana nikaamua kuzizuia simu za huyu (Q Boy) hadi nimaliziwe pesa yangu.
Hata hivyo, katika sakata hilo ilielezwa kuwa Shilole na Q Boy hawakuwa na makubaliano yoyote kuhusu shoo hiyo na simu hizo hivyo madai ya mwigizaji huyo ni ‘usanii’ tu.

MAMA DIAMOND AINGILIA KATI KUOKOA
Zogo hilo lilipopamba moto na kuashiria kuvurugika kwa amani, mama mzazi wa Diamond, Sanura Kasim ‘Sandra’ aliamua kuingilia kati na kuagiza suala la kudaiana simu lifanyike kesho yake (Jumamosi) kwa vile siku hiyo haikuwa muafaka.
“Jamani! Jamani! We nani, Shilole na we Majaliwa, naomba kwa leo muepusheni shetani kwani hapa si mahali pake, ila kesho tutaitana na kumaliza suala hili, mimi mwenyewe nitalisimamia,” alisema bi mkubwa huyo na kumaliza henyahenya iliyoibuka.

JUMAMOSI YAFIKA, KIKAO VIPI?
Jumamosi, mapaparazi wetu walifuatilia ishu hiyo nyumbani kwa akina Diamond na kuulizia ili kujua kama kikao cha usuluhishi kilifanyika kama mama Nasibu alivyoagiza.
“Mh! Sijaona kikao chochote, kwanza Shilole mwenyewe akipigiwa simu hapokei,” alisema ndugu mmoja wa Diamond huku akiomba hifadhi ya jina lake.

MSIKIE DIAMOND
Juzi, Diamond alipopigiwa simu na kuulizwa kama anaijua ishu ya simu, alikubali.
Staa huyo alisema anashindwa kuingilia kati sakata hilo kwa sababu wahusika wote ni watu wake wa karibu kikazi.
“Yeah! Ishu ni kweli ipo, lakini mimi nilijiweka kando mapema, nikamwambia dogo (Q Boy) afuatilie mwenyewe baada ya kuona Shilole haeleweki.
“Unajua Shilole ni mwanamuziki mwenzangu, dogo yupo ndani ya Kampuni ya Wasafi Entertainment (ya Diamond), sasa kukomaa na ishu za simu tu nahisi itanishushia hadhi, napiga shoo za hela nyingi halafu leo nakomaa kwa hela ndogo, inakuwa siyo,” alisema Diamond.

SHILOLE TENA
Baada ya kuzungumza na Diamond, Shilole alipigiwa simu na kuomba kufafanua kwa undani ishu hiyo ambapo katika hali isiyotarajiwa, alimlalamikia paparazi wetu akidai anapendelea katika sakata hilo.
“Nyiye mnamtetea tu yule dogo, mimi sina tatizo, kama rafiki yake (aliyemuitia shoo Afrika Kusini) akinilipa hela yangu nawapa simu zao,” alisema Shilole.
Msanii huyo alikwenda mbele zaidi kwa kumwambia paparazi kuwa atatia timu kwenye Ofisi za Global Publishers ili kuzungumzia suala hilo na viongozi.
Baadaye Shilole alifika ofisini kwetu na kufafanua juu ya sakata hilo ambapo alirudia kukiri kuzuia simu hizo akidai kwamba anamdai Q Boy hivyo mpaka atakapomlipa ndiyo atampa simu zake.

Q BOY NAYE TENA
Kwa upande wake, Q Boy alipozungumza na paparazi wetu siku hiyo alisema amekusudia kwenda kufungua kesi kituoni ili apewe msaada zaidi wa kisheria kwa vile simu hizo zinamuuma hasa ukizingatia kuwa yeye siye aliyempeleka Shilole Afrika Kusini kufanya shoo.
“Mimi leo (Jumatatu) nimebanwa sana, kuna sehemu nakwenda na Diamond, nadhani nitamaliza jioni. Lakini kesho (Jumanne) nitaamkia polisi kufungua kesi nione watanisaidiaje?” alisema Q Boy.

POLISI AGUSIA ISHU
Risasi Mchanganyiko lilizungumza na askari mmoja kutoka Kituo cha Polisi cha Oysterbay na kummegea mtiririko wote, kisha kumuuliza kama kuna kesi ambapo alijibu:
“Japokuwa mimi si msemaji wa jeshi (la polisi), lakini ishu kama hiyo shitaka lake lipo, ni wizi wa kuaminiwa. Unajua wengi wanadhani kuibiwa lazima mtu uwe hujui, lakini mtu akifanya kama hivyo alivyofanya huyo msanii nani sijui (Shilole), kama ni kweli, kosa linakuwa wizi wa kuaminiwa endapo atafikishwa polisi.”

DIAMOND, Q BOY WALIFANYA MCHEZO?
Hata hivyo, baadhi ya watu walioshuhudia sakata hilo walikuwa na maswali kibao yaliyokosa majibu.
Swali la kwanza: Shilole alikwenda kufuturu kwa mwaliko wa Diamond na alijua staa huyo na Q Boy ni wamoja na simu alizopewa ilikuwa amletee msanii huyo, kwa nini alikwenda huku akijua ana msala?
Swali la pili: Kama Shilole alikwenda akijua Q Boy hayupo Bongo, je! Si kwamba ulikuwa mpango wa wawili hao kumwita ili wampe kibano ateme simu zao?
Swali la tatu: Je, ni kweli Shilole alizuia simu ili amaliziwe deni lake kwa mtu aliyemuitia shoo Afrika Kusini au shetani alimwingia baada ya kutua Bongo na kuamua kuzitumia hasa ikizingatiwa kuwa siku hizi mambo ya Instagram ndiyo habari ya mjini?

SOURCE: GPL

Read More »

Uwoya Amtuhumu Lucy Komba Kumchukulia Mumewe, Soma Kisa Kizima Hapa!!!


Stori:Imelda Mtema
NYOTA wa filamu za Kibongo, Irene Pancras Uwoya ‘Mama Krrish’ ametoa kali ya mwaka baada ya kudai kwamba amemshika ugoni msanii mwenzake, Lucy Komba mara baada ya kuziona picha za msanii huyo akiwa na mumewe, Hamad Ndikumana ‘Kataut’ wakiigiza filamu.
Lucy Komba anayedaiwa kushikwa ugoni na Irene Uwoya.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi kwa njia ya simu kutokea nchini Swaziland, Uwoya amepinga vikali utetezi unaosemwa kwamba Lucy na Kataut walikuwa wakishuti filamu na anaamini kuwa msanii huyo ameamua kumzunguka na kutaka kuibomoa ndoa yake.
Irene Uwoya anayedai kumshika ugoni Lucy.
“Lazima kuna kitu kinaendelea kwani katika dunia hii sijawahi kuona filamu inayochezwa na watu wawili tu mwanzo mpaka mwisho, ninachotaka kusema  ni kwamba Lucy ana mpango wa kuiharibu ndoa yangu,” alisema Uwoya kwa hasira.
Uwoya amehoji usiri wa filamu hiyo na kila alipokuwa akimpigia simu mumewe alikuwa akimjibu kwamba yuko Rwanda kumbe alikuwa Bongo akiigiza filamu na Lucy.
“Kwanza Lucy ashukuru niko mbali, laiti ningekuwa karibu angenieleza vizuri kwa sababu hata yeye angeweza kunipigia simu na kunifahamisha ushiriki wa mume wangu kwenye filamu hiyo kwa kuwa namba zangu anazo, ilikuwaje hakufanya hivyo?” alihoji.
Kuonesha kwamba amechukizwa na kitendo hicho, Uwoya alisema kwamba akitua Bongo atamtafuta Lucy ili aweze kumshughulikia vizuri na ikiwezekana amuoneshe hiyo filamu waliyoigiza watu wawili tu.
“Nitatua Bongo siku si nyingi na cha kwanza ni kumtafuta Lucy, anieleze vizuri kuhusu filamu hiyo waliyocheza na mume wangu,” alisema Uwoya.
Filamu hiyo ambayo imekuwa maumivu makubwa kwa Uwoya, imechezwa na Lucy na Ndikumana tu mwanzo hadi mwisho na imepewa jina la Kwa Nini Nisikuoe.


SOURCE: GPL

Read More »

Askari 117 washindwa kumaliza Mafunzo, Sababu zikiwa ni Utoro, Utovu wa Nidhamu na Matatizo ya Afya.



Wanafunzi 117 wa Polisi, wamefukuzwa katika Chuo cha Taaluma na Mafunzo ya Polisi (MPA), kilichopo Manispaa ya Moshi, mkoani Kilimanjaro.
Waliotupiwa virago na kufutwa kwenye kozi hiyo ni wale waliopoteza sifa za kuendelea na mafunzo ya kijeshi baada ya kukutwa na makosa ya utovu wa nidhamu, utoro na matatizo ya kiafya.
Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP), Matanga Mbushi, ambaye ni mkuu wa chuo hicho aliliambia NIPASHE katika mahojiano maalumu kwamba, waliotimuliwa chuoni ni kati ya askari wanafunzi 3,189 waliokuwa wamesajiliwa kuanza mafunzo ya kijeshi katika chuo hicho, Oktoba 25 mwaka jana.
Kati yao askari 115 ni wale wa Polisi na askari wawili wanatoka katika Idara ya Uhamiaji iliyopo chini ya Wizara ya Mambo ya Ndani.
Kufukuzwa kwa wanafunzi hao , kuna akisi moja kwa moja jinsi menejimenti ya chuo hicho ilivyojipanga upya kupunguza wimbi la baadhi ya askari walioko kazini na ambao wanalipaka matope jeshi hilo kutokana na kupotoka kimaadili kwa kutaka kujinufaisha kimaslahi.
Askari hao walikuwa waungane na wenzao ambao wanatarajiwa kuhitimu mafunzo ya awali ya polisi na uhamiaji, Julai 26 mwaka huu baada ya kupatiwa mafunzo ya medani za kivita. Mgeni wa heshima atakayeshuhudia kuagwa kwa askari 3,092 ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk. Emmanuel Nchimbi.
Kamishna Mbushi alisema askari hao pamoja na mambo mengine wamepatiwa mafunzo maalumu ya utunzaji wa amani ya nchi iliyopo, Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (ICT), Haki za Binadamu, Masuala ya mtambuka (Cross cutting issues), Usimamizi wa majanga na Usimamizi wa kazi za Polisi.
Mafunzo mengine ni pamoja na Polisi Jamii, Sheria ya ushahidi, Sheria ya mwenendo wa makosa ya jinai, Upelelezi wa makosa ya jinai, Usalama barabarani na stadi za kazi.
Taarifa za awali kutoka ndani ya chuo hicho, zinaeleza kuwa mahafali hayo ya Polisi yatatanguliwa na medani za kivita yatakayofanyika Julai 25 huko katika Kijiji cha Kilele-Pori, Wilaya ya Siha
  Source: Swahilitz

Read More »

Dah!! Kumbe Nay wa Mitego Mtoto wa Mama!!!


Mkali wa Muziki gani, True Boy Ney wa Mitego, Mzee wa Mkong'oto Jazz Band, alikutwa na Kamera ya Paparazi akiwa kajiachia katika mapaja ya mama yake mzazi huko maeneo ya kwao, kwa picha hii tunapata ukweli wa ule usemi usemao" Mtoto kwa Mama ....." Hata uwe Mbabe na Njemba Kiasi gani, Kwa Mama Utapiga Kimya kama asemavyo Ney.


Picha Credit: GPL

Read More »

Mlemavu wa Miguu amvua Papa Mwenye Kilo zaidi ya 250.


Kijana Mlemavu wa miguu, Matt Sechrist, 19 juzi aliandika kumbukumbu ya maisha yake baada ya kumkamata Papa mwenye uzito wa zaidi ya kilo 250 katika Fukwe za Vilano huko Florida.

Matt alifanikiwa kumkamata Papa huyo akisaidiwa na Baba yake pamoja na Rafiki wa Babab yake, Iliwachukua takribani saa moja kuhangaika na kiumbe huyo mpaka kumtoa nchi kavu, hata hivyo baada ya kupiga nae(Papa) picha za ukumbusho pamoja na watu wengine walimrudisha katika maji.

Read More »

Mbaroni kwa Unyanyasaji na Utesaji wa Panya, Mijusi na Nyoka 20,000.

-->

Waokoaji huko LOS ANGELES Marekani wamefanikiwa kuwaokoa zaidi  ya Panya, Mijusi na Nyoka 20,000 ambao walikuwa katika hali mbaya na hatarani kufa katika stoo moja maalum ya kufugia wanyama.

Mitchell Steven Behm (l.), 54, the owner of Global Captive Breeders in Lake Elsinore, Calif. Behm and company manager David Delgado, also known as Jose Magana (r.), 29, have been charged with more than 100 counts each of felony animal cruelty for the way they treated many of nearly 20,000 rats and reptiles found dead, dying or diseased at a breeding center in Lake Elsinore, authorities said Monday.

Mitchell Steven Behm (Kushoto), 54, Mmiliki wa Global Captive Breeders huko Lake Elsinore, Calif. Behm na Meneja David Delgado, au Jose Magana (Kulia), 29,

Taasisi maalum ya kulinda na kutetea haki za wanyama ilipigiwa simu na msamaria mwema kuhusu kuteswa na kuwekwa katika mazingira mabaya hadi kufa kwa wanyama hao, hivyo walimtuma mpelelezi katika stoo hiyo na kujifanya anaomba kazi ya utunzaji wanyama.

 This Dec. 2012 photo provided by People for Ethical Treatment of Animals (PETA) shows flooding rat enclosures and spilling water onto a facility floor where rats were warehoused like shoes in rack after rack of tiny tubs, at a breeding center in Lake Elsinore, Calif.


 Alifanikiwa kupata kazi na ndipo alipoweza kufanya uchunguzi zaidi na kukusanya ushahidi wa kutosha uliopelekea watuhumiwa hao kusomewa mashtaka zaidi ya 100 ya unyanyasaji na uvunjaji wa haki za wanyama.
 Riverside County authorities say two men have been charged with 106 counts of felony animal cruelty for the way they treated nearly 20,000 rats and reptiles found diseased, dying or dead. (AP Photo/PETA)

Read More »

Join Swahili One Community, "Like" and you will be one of us forever

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...
Copyright © 2013. swahili one Blog - All Rights Reserved
Customized by: Grace Tommy The One | Powered by: BS
Designed by: Creative Blogger